MKUU wa Mkoa Rukwa Charles Makongoro Nyerere ameipongeza halmashauri ya Wilaya ya Nkasi kwa kupata hati safi na kuwa hicho ni kielelezo cha ushirikiano mzuri kati ya watendaji wa halmashauri ,madiwani na wadau wengine katika kuona halmashauri inasonga mbele.
Pongezi hizo amezitoa leo Juni 11,2025 kwenye kikao maalumu cha Baraza la Madiwani kuhusu utekelezaji wa hoja za ukaguzi na mapendekezo ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali kwa mwaka 2023-24 ambapo amesema kuwa katika msimu uliopita kulikua na hoja nyingi za ukaguzi lakini kwa sasa zimepungua mno na kuona kwamba kuna kitu kinafanyika ndani ya halmashauri.
Amesema kuwa amefurahishwa na namna ambavyo imekuwa ikijishughulisha na ufutaji wa hoja mbalimbali zilizojitokeza kwa kutolea mfano kuwa kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Aprili 2025 halmashauri ya wilaya Nkasi ilionyesha kuwa na hoja za miaka ya nyuma 21 na hivyo kufanya kuwa na hoja 38 na maagizo 4 yenye vipengele 10 ya kamati ya kudumu ya bunge ya hesabu za serikali (LAAC) ambapo maagizo hayo mengi yapo katika ya utekelezaji na hoja nyingi kufutwa.
Kufuatia hali hiyo Mkuu huyo wa Mkoa amependa kusisitiza baadhi ya hoja ambazo inatakiwa kufanyika kwa haraka kuwa ni mwenendo wa ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa mwaka 2023/24,usimamizi wa manunuzi na miradi ya maendeleo,usimamizi wa Rasilimali watu na mali za halmashauri,usimamizi wa matumizi ,upimaji wa ufanisi na utekelezaji wa mpango na bajeti.
Nkasi District Council
Anwani ya posta: P. O. Box 2, Namanyere - Nkasi
Simu: +255252830006
Simu ya mkononi: +255252830006
Barua pepe: ded@nkasidc.go.tz
Haki miliki