• malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi. |
Nkasi District Council
Nkasi District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

  • Nyumbani
  • Kuhusu sisi
    • Dhima na Dira
      • Muundo wa Taasisi
    • Muundo wa Taasisi
    • Historia
  • Utawala
    • Idara
      • Idara ya Fedha
      • Utawala na rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Maendeleo ya jamii
      • Elimu msingi.
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na mitambo
      • Ardhi na maliasili
      • Kilimo na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA
    • Muundo wa taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa kwa umma
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Nyuki

Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi ina misitu ya asili 15 inayokadiriwa kuwa na ukubwa wa hekta 3,014 na pia kuna mito mikubwa na midogo isiyokauka kwa kipindi chote cha mwaka. Misitu hii ina aina mbalimbali za miti zinazotoa maua yanayowezesha upatikanaji wa asali yenye ubora wa kipekee. Hata hivyo yapo mazao mbalimbali ya chakula na biashara kama mahindi, alizeti, viazi vitamu na miti mingi ya matunda ambayo hutoa maua yanayosaidia katika upatikanaji wa poleni.

Hata hivyo katika kuhakikisha kuwa rasilimali ya nyuki inaendelezwa ili ichangie katika kuinua kipato cha jamii na kushiriki katika utunzaji wa mazingira endelevu, huduma mbalimbali zinatolewa kwa wananchi. Huduma hizo ni pamoja na :- Utoaji wa hamasa na elimu ya ufugaji wa nyuki, Kutoa vifaa vitumikavyo katika ufugaji wa nyuki, ikiwemo mizinga ya kisasa na mavazi ya kurinia kwa vikundi vya wafugaji wa nyuki, Kutoa elimu ya ujasiriamali kwa vikundi vya wafuga nyuki.

Hadi mwezi February/2015, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi ina mizinga ya kisasa ya ufugaji nyuki ipatayo 1,363 ya kisasa na 4,648 ya kienyeji na wafugaji wa nyuki wapatao 357 na idadi hii inazidi kuongezeka kutokana na hamasa inayoendelea kutolewa.

UFUGAJI WA NYUKI

Ufugaji wa nyuki ni taaluma inayotumia rasilimali ya nyuki (wanaouma na wasiouma) na mimea katika kuzalisha asali, nta, gundi ya nyuki, maziwa ya nyuki, majana, sumu ya nyuki, chavua na nyuki wenyewe.

FAIDA ZA UFUGAJI NYUKI

Mdau wa ufugaji wa nyuki anaweza kufaidika na taaluma hii kama vile:-

  • Kuongeza pato lake na jamii yake.
  • Kuhifadhi mazingira yanayozunguka eneo analoishi.
  • Kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula kwani nyuki huchavusha mimea wakati akitafuta chavua.
  • Huongeza ubora wa matunda na mbegu za mimea kutokana na uchavushaji.
  • Hutunza ikolojia na kuhifadhi bioanuai za wanyama na mimea katika eneo husika .
  • Shughuli ya ufugaji wa nyuki huweza kufanywa na mtu mwenye hali, umri na jinsia yoyote (mlemavu, mzee au kijana).
  • Mazao ya nyuki yaweza kuwa malighafi kwa viwanda vingine vidogovidogo kama vile nta hutumika katika viwanda vya kutengeneza mishumaa, sabuni na vipodozi.
  • Upatikanaji wa ajira kwa vijana, wanawake na wazee.

 

FURSA ZA UFUGAJI NYUKI ZILIZOPO

  • Uwepo wa misitu ya hifadhi inayofaa kwa ufugaji wa nyuki.
  • Upatikanaji wa vyanzo mbalimbali vya maji kama vile mabwawa na mito mikubwa na midogo inayotiririsha maji katika kipindi kirefu cha mwaka.
  • Uwepo wa nguvukazi ya kutosha na utayari wa wananchi kufuga nyuki.
  • Uwepo wa Sera ya Taifa ya ufugaji nyuki ya mwaka 2002, sheria ya ufugaji nyuki na kanuni zake.
  • Upatikanaji rahisi wa makundi ya nyuki, hususani wanaouma, katika maeneo mbalimbali ya mji wetu.
  • Uwepo wa kilimo cha mazao ya chakula na biashara, kilimo cha miti ya matunda ambayo huwezesha upatikanaji wa asali iliyo nzuri.

CHANGAMOTO ZINAZOKABILI KITENGO CHA NYUKI

  • Uvamizi na uchomaji ovyo wa misitu kutokana na shughuli za kilimo.
  • Kutokuwa na elimu ya kutosha kuhusu ufugaji wa kisasa wa nyuki.
  • Ukosekanaji wa mitaji kwa wafugaji kwa ajili ya kuendesha shughuli hii.
  • Uzalishaji mdogo wa asali kukidhi soko la ndani na la nje ya nchi.
  • Uhaba wa upatikanaji wa vifaa maalum kwa ajili ya shughuli za ufugaji nyuki, mfano vifaa na mavazi ya kinga.
  • Uhaba wa wataalam katika sekta hii.

Matangazo

  • TANGANZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 04, 2025
  • Onesha zote

Taarifa mpya

  • KAMATI YA AFYA MSINGI WILAYA YA NKASI

    April 23, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WAPEWA MAFUNZO YA MFUMO WA IFTMIS

    April 15, 2025
  • Onesha zote

Video

HOTUBA YA MH.MKUU WA WILAYA NKASI
Video za hivi punde

Ukurasa wa karibu

  • Utumishi wa umma
  • Ofisi ya Rais,Tawala za mikoa na serikali za mitaa
  • Mfumo wa manunuzi nest
  • Employee Self Service

Kurasa zinazofanana.

  • Tovuti ya mkoa wa Rukwa
  • Wizara ya elimu sayansi na teknolojia
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la mitihani
  • Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia
  • Wizara ya mambo ya ndani ya nchi.
  • Wizara ya Kilimo
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Utumishi Portal

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Nkasi District Council

    Anwani ya posta: P. O. Box 2, Namanyere - Nkasi

    Simu: +255252830006

    Simu ya mkononi: +255252830006

    Barua pepe: ded@nkasidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Haki miliki