• malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi. |
Nkasi District Council
Nkasi District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

  • Nyumbani
  • Kuhusu sisi
    • Dhima na Dira
      • Muundo wa Taasisi
    • Muundo wa Taasisi
    • Historia
  • Utawala
    • Idara
      • Idara ya Fedha
      • Utawala na rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Maendeleo ya jamii
      • Elimu msingi.
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na mitambo
      • Ardhi na maliasili
      • Kilimo na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA
    • Muundo wa taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa kwa umma
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wafugaji wilayani Nkasi Washauriwa kuunda Ushirika

Imewekwa tarehe: December 7th, 2017

Wafugaji kupitia umoja wao wa Wafugaji wilayani Nkasi mkoani Rukwa wameshauriwa kuunda ushirika utakaowawezesha kujenga mtaji mkubwa na kuweza kuanzisha kiwanda cha kuchakata bidhaa mbalimbali zitokanazo na mazao ya mifugo na kuweza kujikwamua kiuchumi.

Ushaurio huo umetolewa jana na afisa ushirika wa mkoa Rukwa Wales Kilia kwenye mkutano mkuu wa umoja wa Wafugaji wilayani Nkasi ambapo alidai kuwa Wafugaji katika umoja wao huo wanao uwezo mkubwa wa kuanzisha ushirika mkubwa utakaowawezesha kutengeneza mtaji mkubwa na kugeuka na na kuwa wawekezaji kupitia viwanda.

Alisema katika taarifa aliyosomewa na katibu wa umoja umoja huo  jinasa Bilia ni kuwa umoja huo wenye wanachama 159 kwa muda wa miaka mitatu iliyopita walikua na hakiba ya Tshs,Mil.12 lakini hadi kufikia sasa wameweza kufikisha Mil.35 na kuwa mtiririko huo kama wataugeuza umoja huo na kuwa ushirika wanaweza wakafika mbali zaidi.

Alisema katika taarifa hiyo ameona kipengele ambacho wafugaji wameiomba serikali kuwatafutia wawekezaji na kuwa sasa wao wenyewe wanaweza wakawa wawekezaji kwa kuanzisha kiwanda kikubwa ambacho mwisho wa siku kitawatoa katika lindi la umasikini ikiwa ni pamoja na kuongeza ajira kwa vijana wao.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya tatu imejielekeza kwenye uchumi wa kati ambao ni wa viwanda na kuwa jambo hilo linawezekana kama wao wataweza kujenga ushirika wenye nguvu na kuwa ushirika utawafanya wao waweze kukopesheka kwenye taasisi mbalimbali za kifedha na kuwa viwanda ni kitu cha kawaida ambacho kinaweza kikaanzishwa na mtu yeyote na kuondoa mawazo kuwa wawekezaji pekee ndiyo wenye uwezo wa kuwekeza viwanda.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya Nkasi Julius Kaondo kwa upande wake aliwatoa wasiwasi wafugaji hao juu ya uanzishwaji wa ushirika na kuwa yeye sasa atawasaidia Wafugaji hao walau kuweka kituo cha kukusanyia maziwa ili wanunuzi waweze kuwakuta hapo na hata ikibidi atamfuata mwekezaji wa kuwekeza katika sekta hiyo ya Maziwa ambalo ni moja ya mazao yatokanayo na mifugo yao.

Alisema kuna baadhi ya changamoto nyingi ambazo serikali inabidi izifanyie kazi na kuwa amezisikia na zile alizo na uwezo nazo atahakikisha anazitafutia ufumbuzi wa haraka

Mwenyekiti wa umoja huo Msemakweli Msalaba alidai kuwa wazo hilo wamelichukua na kuwa watalifanyia kazi haraka sana na kuhakikisha kuwa wanaanzisha ushirika mkubwa na wenye nguvu ambao pia utakua ni wa kupigiwa mfano.

Na aliiomba serikali iwe inatoa elimu kwa wafugaji juu ya matumizi bora ya ardhi,ikiwa ni pamoja na namna ya kuitumia mifugo waliyonayo katika kuweza kujiletea maendeleo badala ya kuona fahari ya kuishi nas mifugo mingi isiyokuwa na tija

Matangazo

  • KAZI ZA MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI KWA MWAKA HUU 2022 May 06, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NA KATIBU MAHSUSI III May 26, 2022
  • Onesha zote

Taarifa mpya

  • Serikali wilayani Nkasi mkoani Rukwa imeteketeza TANI mbili ya samaki wakavu waliobainika kuhifadhiwa kwa kutumia sumu

    July 19, 2019
  • Mwenge wa Uhuru unatarajia kuzindua na kuweka mawe ya msingi katika miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani Nkasi yenye thamani ya zaidi Tshs,Bil.29

    April 07, 2019
  • Siri kubwa ya kudumisha vikundi vya VICOBA hii hapa

    October 11, 2018
  • Kupuuzwa kwa baadhi ya mila na desturi ni miongoni mwa sababu zinazochangia ongezeko la mimba za utotoni

    October 11, 2018
  • Onesha zote

Video

Ziara ya Waziri Mkuu Wilaya ya Nkasi
Video za hivi punde

Ukurasa wa karibu

  • Utumishi wa umma
  • Ofisi ya Rais,Tawala za mikoa na serikali za mitaa

Kurasa zinazofanana.

  • Tovuti ya mkoa wa Rukwa
  • Wizara ya elimu sayansi na teknolojia
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la mitihani
  • Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia
  • Wizara ya mambo ya ndani ya nchi.
  • Wizara ya Kilimo
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Utumishi Portal

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Nkasi District Council

    Anwani ya posta: P. O. Box 2, Namanyere - Nkasi

    Simu: +255252830006

    Simu ya mkononi: +255252830006

    Barua pepe: ded@nkasidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Haki miliki