• malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi. |
Nkasi District Council
Nkasi District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

  • Nyumbani
  • Kuhusu sisi
    • Dhima na Dira
      • Muundo wa Taasisi
    • Muundo wa Taasisi
    • Historia
  • Utawala
    • Idara
      • Idara ya Fedha
      • Utawala na rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Maendeleo ya jamii
      • Elimu msingi.
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na mitambo
      • Ardhi na maliasili
      • Kilimo na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA
    • Muundo wa taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa kwa umma
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MAADHIMISHO YA WIKI YA ELIMU YA WATU WAZIMA NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI

Imewekwa tarehe: September 2nd, 2025

Watu wazima ambao hawakufanikiwa kupata elimu kupitia mfumo rasmi wametakiwa kuichangamkia fursa ya elimu inayotolewa nchini kote bila kujali umri wao na aibu,  kwani upo utaratibu mzuri wa wao kufundishwa.

Hayo yamebainishwa leo September 2, 2025, na mkuu wa wilaya ya Nkasi ambaye pia alikuwa mgeni rasmi, katika sherehe za kilele Cha maadhimisho ya wiki ya elimu ya watu wazima Peter Ambrosi Lijualikali, zilizofanyika katika viwanja vya chuo Cha VETA Paramawe Halmashauri ya wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa ,huku akitoa wito kwa watu wote kuishika elimu na kuipigania.

Aidha katika kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika oktoba 29, mwaka huu Lijualikali amewasisitiza wananchi kudumisha amani umoja na mshikamano kama taifa pamoja na kufanya kampeni kistaarabu.

"Nafahamu hapa wengi mmejiandikisha na zoezi lilifanyika vizuri nafahamu, Kila mtu ana chama chake, tunawagombea mbalimbali kuanzia ngazi ya udiwani, ubunge na urais, ombi langu kwenu nikuendelea kudumisha amani umoja na mshikamano kama taifa tukafanye kampeni za kistaarabu, tukawafanyie tunaowataka lakini pia tukawaheshimu tusiowataka" amesema Lijualikali.

Awali akisoma taarifa  mbele ya mgeni rasmi Afisa elimu ya watu wazima  Sekondari na elimu nje ya mfumo rasmi  Thomas Mhagama kwa niaba ya Afisa elimu ya watu wazima Msingi na nje ya mfumo rasmi  Jesca Lwiza  amesema kuwa chimbuko la maadhimisho ya elimu ya watu wazima yalianza mwaka 1975, ambapo hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliona ni vyema watu wake wapate elimu kwani idadi kubwa kwa wakati huo walikuwa hawajui kusoma Wala kuandika.

Kupitia taarifa hiyo Mhagama amesema Tanzania kama ilivyo nchi nyingine duniani imekuwa ikiadhimisha juma la elimu ya watu wazima Kila mwaka shabaha yake kuu ni kuhamasisha jamii nzima kutambua nafasi ya elimu kwakila mtu bila kujali umri, jinsia na hali ya maisha, na hii ikidhihirisha kuwa elimu ni endelevu na haina kikomo na ni urithi wakudumu kwamaendeleo ya mtu binafsi na Taifa kwa ujumla.

Akisoma hotuba kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Nkasi, mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Afraha Hassani amesema kuwa dhana ya kukuza kisomo katika dhama za kidigitali imekuja kwasababu katika maisha kwenye jamii , mazingira yamebadilika, hali ya hewa imebadilika, mifumo ya Kiuchumi imebadilika, hali ya milipuko ya magonjwa inaongezeka nakudai kuwa vyote hivi vinaitaka jamii iendelee kusoma ili kupata elimu ya kukabiliana navyo bila kujali utoto hadi utu uzima, hivyo jamii ibadilike iendane na sayansi na Teknolojia.

Aidha alifurahishwa na mwamko mkubwa wa vyuo wilayani Nkasi katika kushiriki maadhimisho ya wiki ya elimu ya watu wazima ambayo yameletwa mwamko mkubwa kwa jamii kwenda kujifunza.

" Nimefurahi kuona mwamko mkubwa wa vyuo vyetu wilayani Nkasi kuja kushiriki maadhimisho haya ya wiki ya elimu ya watu wazima ambayo kimsingi yameletwa mwamko kwa jamii kuja kujifunza" alisema mkurugenzi huyo.

Sambamba na hayo ameagizi Kila  Kijiji na kitongoji ambacho kina watu wazima wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu, kuhakikisha madarasa ya watu wazima yanafunguliwa, na kusisitiza kua wanafunzi waliocha shule kwa sababu mbalimbali ikiwemo ujauzito warudi shule kuendelea na masomo ili watimize ndoto zao.

Maadhimisho hayo ya kilele cha wiki ya elimu ya watu wazima yalipambwa na maonesho ya fani mbalimbali kutoka katika vyuo na taasisi za serikali na zisizo za serikali huku yakisindikizwa na kaulimbiu isemayo " kukuza kisomo katika zama za kidigitali kwa maendeleo endelevu ya Taifa letu"

Matangazo

  • TAARIFA YA MAFUNZO ELEKEZI KWA WALIMU WALIOAJIRIWA KATIKA UTUMISHI WA UMMA 2025 July 09, 2025
  • Onesha zote

Taarifa mpya

  • MAADHIMISHO YA WIKI YA ELIMU YA WATU WAZIMA NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI

    September 02, 2025
  • MASHINDANO YA RIADHA YATIMUA VUMBI LEO SHIMISEMITA TANGA

    August 21, 2025
  • Onesha zote

Video

HOTUBA YA MH.MKUU WA WILAYA NKASI
Video za hivi punde

Ukurasa wa karibu

  • Utumishi wa umma
  • Ofisi ya Rais,Tawala za mikoa na serikali za mitaa
  • Mfumo wa manunuzi nest
  • Employee Self Service

Kurasa zinazofanana.

  • Tovuti ya mkoa wa Rukwa
  • Wizara ya elimu sayansi na teknolojia
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la mitihani
  • Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia
  • Wizara ya mambo ya ndani ya nchi.
  • Wizara ya Kilimo
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Utumishi Portal

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Nkasi District Council

    Anwani ya posta: P. O. Box 2, Namanyere - Nkasi

    Simu: +255252830006

    Simu ya mkononi: +255252830006

    Barua pepe: ded@nkasidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Haki miliki